Friday, May 24, 2013
NATOA ZAWADI KWA WASOMAJI WANGU WOTE WA DJCHOKAblog MLIOKO KOTE DUNIANI.
Kama wewe ni mtembeleaji wa DJCHOKAblog basi naomba hivi ukibahatika kuwa mtembeleaji wa blog na pembeni ukaona ile views imeonyesha 7000000 naomba uipige picha halafu unitumie hiyo picha kwenye email yangu hii djchoka84@yahoo.com kama unavyoiona picha hii hapa nilivyofanya au kwa njia yako yoyote ile.
(News) MKALI WA VODACOM:
Je,
unajiamini kuwa na kitu kinachokufanya uwe mkali mtarajiwa? Vodacom
inatafuta mtangazaji mpya wa kipindi cha TV kitakachoanza hivi karibuni.
Soma namna ya kushiriki na unaweza kuwa mmoja ya watangazaji wa kipindi
hiki.
Kazi ni kwako.
Labels:
News,
Vodacom Tanzania
(Album Cover & Audio) HII NDIO ALBUM YA KATO BY WAKUVWANGA (ORIJINO KOMEDI)
Ningependa
kuchukua fursa hii kukushirikisha kwenye kampeni yetu ya kwanza kutka
kampuni hii ambayo inahusisha usambazwaji wa DVD za album ya kwanza ya
Wakuvwanga inayojulikana kama
KATO.Album hii inatarajiwa kuzinduliwa na kuanza kuuzwa tarehe 31st May
2013 siku ya ijumaa saa 12 asubuhi,wewe kama mmoja kwenye timu ya
wapiganiaji haki za wasanii na una uwezo wa kuitangaza kazi hii tumeona
tuwasiliane nawe moja kwa moja katika kutoa ujumbe huu kwa wananchi na
wapenzi wako.
tunategemea
kutoa pikipiki 5 wakati wa uuzaji huu ambazo zitapatikana kwa mtu
yeyote ambaye atapata bahati ya kununua DVD yenye label ya pikipiki
ndani.Tutakuwa na magari 5 abayo yatazunguka mji wa Dar Es Salaam kwa
siku zote tatu kwa wananchi watakaonunua rejareja(ijumaa,jumamosi na
jumapili) na kwa watakaotaka kununua kwa jumla watatakiwa kupika simu
zifuatazo na kupewa maelekezo ya wapi kwenda kulipia mzigo watakaotaka
na kuupata.
0656-621807 Famy
0718-852828 Waku
0717-792023 Mwasu
Tumeshatoa video 2 (angwisa na vatu) na audio zake kufanyia promotion hii.
Labels:
Music,
Wakuvwanga
Thursday, May 23, 2013
(News) Ethiopian Airline wadhamini wa usafiri wa Anga ZIFF 2013 na Skylight Band Kutumbuiza
Kampuni ya usafiri wa anga.. Ethiopian airlines
imejitokeza kudhamini Tamasha la 16 la filamu Tanzania, ZIFF linalotazamiwa
kufanyika Zanzibar, June 29 hadi July 7, 2013. Meneja na Mkurugenzi
msaidizi wa Tamasha hilo Daniel Nyalusi maarufu kwa kifupisho cha Dean alisema wanajisikia
furaha sana kushirikiana na Kampuni hiyo, na kwamba anatarajia ushirikiano huo
utafungua njia kwa makampuni mengine.
(Photo) B.M.F (Bongo Mad Flavaz) Ndani Ya Ambassadors Lounge Ijumaa Hii (24.05.13)
B.M.F
(Bongo Mad Flavaz) Ndani Ya Ambassadors Lounge Ijumaa Hii
(24.05.13),Dullayo,Mirror & Bonge La Nyau Kwenye Stage,Kwenye Wheeks
Kama Kawa Skills/Dj Steve B Na Dj Bulla,Entry 10,000 Kuanzia Saa 3
Usiku...Mpango Ndio Huo
(News) Wakulima sasa kupata taarifa za kilimo kupitia simu
Balozi wa Finland nchini Tanzania, Sinikka Antila akisalimiana na Afisa
maendeleo ya Biashara wa Vodacom Tanzania Nixon Bonaventure wakati wa
hafla ya kuanzisha Ushirikiano kati ya kampuni hiyo na kampuni ya
Sibenonke ya nchini Finland. Pamoja nao katika picha ni Waziri wa
Mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa Alexander Stubb (katikati).
Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala ( wa pili kutoka kushoto)
na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe Schwarz. Hafla hiyo
ilifanyika nyumbani kwa balozi huyo.
Waziri wa mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa wa Finland,
Alexander Stubb, akifanya mahojiano na Meneja Mahusiano wa Vodacom
Tanzania, Bw.Matina Nkurlu katika hafla ya kuingia katika Ushirikiano
utakao wawezesha wakulima kupata taarifa za kilimo kupitia simu za
mkononi. Pamoja nao ni Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala
(wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe
Schwarz.
Labels:
News,
Vodacom Tanzania
(Audio) Last Warning - Nyinda Nyinda
Last Warning Ni kundi lenye maskani yake Arusha Tanzania wanakuja na
ngoma mpya toka Noizmekah studios pini linaitwa Nyinda Nyinda
Labels:
Music
(Introducing) DJ SAM MARK New DJ in town
Anajulikana kwa jina lakutafutia ugali DJ SAM MARK, ni DJ mpya machoni mwa wabongo ila Sam yeye udj alijifunzia kule kwa wenzetu Nairobi Kenya kwenye Academy moja inayoitwa Mixx Master. Ila kwa sasa yupo hapa mjini na mnaotembelea Club Bilicanas basi mnaweza kusikia milazo ya DJ SAM MARK hapo ila anasema yupo Bills kwa muda na mbali na udj pia kwa sasa anatengeneza Mix Tape za video so mkae mkao wa kuziona DVD Mix Tape hizo.
Unaweza kumcheck DJ Sam Mark kwenye mitandao ya kijamii kama
Facebook/djsam mark
Twitter/djsammark
Labels:
DJ Sam Mark,
News
Wednesday, May 22, 2013
(News) Mwana FA awataka wanaume kubadili mtazamo kuhusu fistula
Msanii
mahiri wa kizazi kipya Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA ambae ni
Balozi wa Chapa Vodacom amesema hadhi na heshima ya mwanaume katika
jamii itakuwa
na uzito mbele ya uso wa jamii kwa wao kuwa tayari kutafuta suluhu ya
changamoto zinazoikabili jamii na wala si vinginevyo.
(Photo) IZZO BIZNESS ndani ya CLUB VIBE Mbeya mwisho wa mwezi huu
Kwa wakazi wote wa Mbeya na mashabiki wa Izzo Bizness mtoto wenu atashuka hapo siku ya tarehe 31 katika ukumbi wa CLUB VIBE akiwa ameambatana na wasanii wenzake kwa kiingilio cha elfu 7 tu.
Labels:
Advertising,
Club Vibe Mbeya,
Izzo B
Tuesday, May 21, 2013
(Photo's) Jiachie na camera ya DJCHOKAblog at SAMAKI SAMAKI Mlimani City
Jana msanii wa bongo fleva ambaye nyota yake ilitokea kwenye shindano la Bongo Star Search hapa namzungumzia BELLA KOMBO alikuwa anasherehekea siku yake yakuzaliwa pande ya Samaki Samaki Mlimani City. Ilikuwa ni Dinner Party akaalika washkaji zake kadhaa na kula nao kwa pamoja na siku ikaishia hapo.
(News) Hawa ndio wasanii waliojiunga kwenye chama cha CHADEMA.
Mh Joseph Mbilinyi aka SUGU akiwa na Prof Jay
K wa Mapacha kushoto nae ni moja ya wasanii waliojiunga CHADEMA.
Labels:
k wa mapacha,
News,
prof jay
(Audio) PDC Crew aka Pinda Da Chronics - Long Time
PDC Crew aka Pinda Da Chronics Kundi linaloundwa na LeeShu, Medic,
KingNdela na ElevenOne toka pande za Sombetini Arusha Tanzania wanadrop
joint mpya "Long Time" liloundwa na Producer Black na mix kufanyika Noizmekah Studio chin ya defxtro, pata kusikiliza HAPA na kwa mawasiliano zaid chek na PDC kupitia +255 714 283 324 .Powered by www.vmgafrica.com
Labels:
Music
Sunday, May 19, 2013
AFRO URBAN PARTY EAST MEETS WEST
AFRO URBAN PARTY EAST MEETS WEST..Bring your friends along to this
memorable event..Calling ALL AFRICAN UNDER ONE ROOF in the South of the
UK. Djs bringing you the best mix of Music from the Motherland. Its
going to be heavy..so make a date and don't be late.. See You there
People..!DAMAGE IS £5 ONLY BEFORE 11PM MORE AFTER
Labels:
Advertising
(Audio) Huu ni wimbo maalumu wa kuamasisha ugonjwa wa FISTULA umeimbwa na baadhi ya wasanii wa kike TANZANIA.
Wimbo wa kuamasisha ugonjwa wa FISTULA wa wanawake kwamba kwa sasa unatibika …umeimbwa na baadhi ya wasanii wa kike wote tanzania.>
MWASITI, VUMILIA ,DAYNA, RECHO, THE TRIO, LINAH, MAUNDA ZORRO, MENINAH, FEZA KESSY, KEYSHA, VIDA, PIPI, VANESSA MDEE, QUEEN DARLEEN, ZUHURA, BABY J, SUNDY GAGA= toa sapoti kwa kuamasisha wimbo kwamba FISTULA inatibika,Ahsante
Studio= SURROUND SOUND
Prd= NASH DESIGNER
Phone =0715973697 Au 0717802211
Labels:
baby j,
Dayna,
Feza Kessy,
keysha,
linah,
Maunda Zorro,
Meninah,
Music,
Mwasiti,
Pipi,
Queen Darleen,
Recho,
sundy gaga,
The Trio,
Vanessa Mdee,
vida,
Vumilia,
zuhura
(News) ZIFF yatangaza Filamu zilizochaguliwa
The 16th ZIFF official selection has just been announced. A total of 80 films are featured in 4 categories:
ZIFF Competition, Sembene Prize, Bongo Movies, Out of Competition.
The festival kicks off on 29th June until 7th July.
Here's the complete selection of ZIFF 2013 films including the country and the director for easy reference.
(Official Video) Amour Genius - Bongo Movie
Artist : Amour Genius
Filmed, Edited & Directed By Jerry Mushala
Track : Bongo Movie
Prod. : Fundi Samweli
Labels:
Video
(Cheka na KITIME) ANACONDA KUMPA KIJITI ANANENEPA
Watafiti makini
wa hii blog isiyo makini ambayo inakoelekea ni wazi kubaya maana maelfu
ya
wasomaji wa blog hii iko siku watagoma kabisa kusoma chochota kilicho
humu
labda wawe wanalipwa kwa dola, watafiti wamegundua kitu ambacho ingekuwa
blog nyingine
ingejipendekeza na kuziita BREAKING NEWSSSSSSS. Yaani watafiti wa blog
hii ni
kiboko, mi mwenyewe Rais wa blog hii nimewavulia kofia. Baada ya wiki
kadhaa
kusikia mwanamuziki maarufu Binti Machozi akiwa na sifa mpya ya kuitwa
ANACONDA, watafiti waandishi wetu, wamegundua msanii mwingine ambaye
yeye
anajiita ANANENEPA. Msanii huyu ambaye si mpya kabisa amepewa jina hilo
na
mamia ya watu waliogundua kuwa amekuwa habaniwi nyimbo zake, na amekuwa
anapata
kazi nyingi sirikalini , ambako mwenyewe amesema zinatokana na rushwa.
ANANENEPA ambae ametamba kuwa ni msanii ambaye ameenda Ulaya kuliko
Mtanzania
yoyote duniani, pia ameunga mkono watu kupewa vijiti, hasa kwa kuwa
amekuwa
anapata tabu sana kupata vijiti baada ya kula nyama.. Ngoja tuachie hapa
maana
ANANENEPA ametishia kwenda Mahakamani kama tutaendelea kuandika habari
zake. Na
ukichukulia hata jana alienda Mahakamani kusikiliza kesi mbalimbali, na
Jumapili alienda Mahakamani kuangalia majengo tusingependa aende
tena huko....
Labels:
Cheka na Kitime,
News
Saturday, May 18, 2013
(Photo) JCB'S WEDDING PARTY ARUSHA
Msanii wa Hip Hop nchini anayetokea mkoa wa Arusha "JCB" usiku huu kule Arusha ni sherehe ya harusi yake ambayo harusi hiyo waliifunga wiki kadhaa huko nyuma, sasa leo ndio ile sherehe yenyewe ambayo inafanyika pande za BOT iliyopo kule Arusha. Pichani ni JCB akiwa na mke wake anayeitwa Diana Jorgensen pamoja na wasimamizi wao.
Subscribe to:
Posts (Atom)














.jpg)


















4.jpg)





